Manchester City

Majeraha yamuondoa Haaland Norway

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Mar 2023
Majeraha yamuondoa Haaland Norway

Mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland amejiondoa kwenye kikosi cha Norway kwa ajili ya mechi yao ya kwanza ya kufuzu Euro 2024 kutokana na majeraha.

Haaland, 22, alipata tatizo la paja baada ya kufunga hat-trick katika ushindi wa 6-0 wa City dhidi ya Burnley kwenye robo fainali ya Kombe la FA Jumamosi.

Imeelezwa kuwa atakosa mechi za Norway dhidi ya Uhispania na Georgia katika Kundi A.

"Erling alichukua uamuazi huu alipogundua kwamba hangeweza kupigania timu," kocha wa Norway Stale Solbakken alisema.

"Kwa bahati nzuri, tuna vijana wapambanaji, wenye talanta na mshikamano kuhakikisha tunafanya vizuri katika mechi zinazofuata."

Daktari wa timu ya taifa ya Norway Ola Sand aliongeza: "Baada ya kufanya vipimo na uchunguzi jana ilibainika kuwa hatafanikiwa kuwahi mechi dhidi ya Uhispania na Georgia. Ni vyema akapata matibabu katika klabu yake"

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’