Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi March 23 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Mar 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi March 23 2023

Arsenal, Chelsea na Manchester City wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Italia Wilfried Gnonto, 19, kutoka Leeds United. (Gazzetta dello Sport, Via Metro)

Juventus na Napoli ni miongoni mwa vilabu kadhaa vya Italia ambavyo pia vinavutiwa na Gnonto. (90min) 0

Manchester United inaweza kutumia hamu ya Tottenham kumnunua mlinda mlango Mwingereza Dean Henderson, 26, kuwashawishi Spurs kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 29. (ESPN)

Mshambulizi wa Eintracht Frankfurt wa Ufaransa Randal Kolo Muani, 24, ambaye analengwa kwa pauni milioni 105 na Manchester United, amependekeza kuwa yuko tayari kuhama msimu huu. (L'Equipe, Via Mail)

Manchester City wamefufua nia yao ya kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Florian Wirtz, 19. (90min)

Tottenham iko kwenye hatari ya kumkosa meneja wa zamani Mauricio Pochettino msimu wa joto huku Muajentina huyo akiwa juu kwenye orodha ya wanaotamani Real Madrid iwapo kocha wa sasa Carlo Ancelotti ataondoka. (Times)

Chelsea wamekubali kwamba watahitaji kupata hasara kubwa ikiwa wanataka kumuuza mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 29, msimu wa joto. (Football Insider)

Matumaini ya Arsenal na Barcelona kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Martin Zubimendi kutoka Real Sociedad yanaonekana kuisha baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kusema hatarajii kuondoka mwishoni mwa msimu huu. (Mail)

Barcelona wana nia ya kumsajili beki wa Monaco mwenye umri wa miaka 21 Vanderson. (Sport – In Hispanic)

Vilabu kadhaa vimeonyesha nia ya kutaka kumsajili beki wa kushoto Mwingereza Brandon Williams, 22, kutoka Manchester United. (Football Insider)

Kiungo wa kati wa Juventus na Ufaransa Adrien Rabiot, 27, amedokeza kuwa huenda akavutiwa na uhamisho wa kuelekea Liverpool. (Sun)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
3h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
14h ago
READ MORE β†’