Mmiliki wa Ineos Sir Jim Ratcliffe na Mwanabenki wa Qatar Sheikh Jassim wanatazamiwa kuwasilisha zabuni mpya za kuinunua Manchester United baada ya muda wa mwisho kuongezwa kutokana na ombi lao huku kukiwa na mkanganyiko
Wazabuni hao waliambiwa walikuwa na hadi 21:00 GMT siku ya Jumatano kuwasilisha zabuni za pili, zilizorekebishwa
Kulingana na BBC Sport, wawekezaji wengine kadhaa waliopendekezwa walitoa maoni yao yaliyopelekea kuongezwa muda
Haijulikani ni lini tarehe mpya ya mwisho itakuwa. Ratcliffe na Sheikh Jassim ndio wazabuni pekee waliotangazwa hadharani
Hapo awali Jumatano jioni kulikuwa na taarifa kutoka kwa vyanzo vya karibu kuwa wazabuni hao walikuwa wamewasilisha zabuni mpya.
Hata hivyo baadae imebainika kuwa waliomba kuongezwa muda zaidi ili kufanya maboresho ya ofa zao



