Coastal Union

Coastal Union imepania kubaki Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Mar 2023
Coastal Union imepania kubaki Ligi Kuu

Timu ya Coastal Union imeandaa mikakati madhubuti ya kuhakikisha inajikwamua katika nafasi ya hatari ya kucheza michezo ya mchujo (play off) kusaka nafasi ya kubaki Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao

Kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu Bara, timu mbili zitakazoburuza mkia (ya 15 na 16), zitashuka moja kwa moja kwenda kucheza Ligi ya Championship msimu ujao, wakati zitakazomaliza nafasi ya 13 na 14, zitalazimika kucheza mechi za play off ili kuwania kubaki Ligi Kuu.

Ligi Kuu Bara kwa sasa ipo ukingoni zikiwa timu zote zikibakiza michezo mitano kufikia mwisho wa msimu wa 2022/23, isipokuwa Simba na Yanga tu ambazo zimebakisha mechi sita kila mmoja.

Yanga ipo kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 65 ikifuatiwa na Simba 57 huku Singida Big Stars ikifuata kwa alama zake 48 na Azam ikiwa nyuma yake kwa pointi 47.

Costal Union ipo katika nafasi ya 13 ikiwa na alama 26, ambayo ni ya kucheza michezo ya play off.

Afisa Habari wa Coastal Union, Jonathan Tito, amesema wanajipanga ipasavyo kuhakikisha wanafanikiwa kumaliza katika nafasi nzuri kwa kushinda michezo yote iliyobaki.

"Kikosi chetu kimeingia kambini kikitokea mapumziko ya wiki moja baada ya mchezo wetu wa mwisho dhidi ya Singida Big Stars ambao tulitoka sare ya bao 1-1"

"Mchezo wetu unaofuata ni dhidi ya Dodoma Jiji ambao tutacheza katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma, hivyo mwalimu anakiandaa vema kikosi chetu ili tuweze kupata matokeo mazuri," alisema Tito"

"Mchezo wetu utakuwa mgumu kutokana na nafasi tuliyopo kwa sasa, hivyo tunapaswa kujiandaa vizuri."

Michezo iliyobaki kwa Costal Union mbali ya huo dhidi ya Dodoma Jiji, ni dhidi ya Mtibwa Sugar, Ihefu, Azam FC na Simba ambao utakuwa mchezo wa mwisho utakaochezwa Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam

IPP Media

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
8h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
15h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’