Jumla ya tiketi 10,500 zimenunuliwa na wadau mbalimbali kwa ajili ya mashabiki kwenda kuisapoti timu ya Taifa ya Tanzania kwenye mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu Afcon 2023 dhidi ya Uganda ambao utapigwa Jumanne, March 28 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Kampeni hiyo imeendeshwa leo ikimuhusisha Afisa Habari wa TFF Cliford Mario Ndimbo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, Afisa Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe na Afisa Habari wa Azam FC, Hashim Ibwe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wameshiriki kwenye kampeni hiyo ya kuhamasisha mashabiki wamenunua jumla ya tiketi 4000
Wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa klabu za Yanga, Azam Fc na Simba wameshiriki katika kampeni hiyo



