Tiketi Elfu 10 zanunuliwa Stars vs Uganda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd March 2023


Tiketi Elfu 10 zanunuliwa Stars vs Uganda

Jumla ya tiketi 10,500 zimenunuliwa na wadau mbalimbali kwa ajili ya mashabiki kwenda kuisapoti timu ya Taifa ya Tanzania kwenye mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu Afcon 2023 dhidi ya Uganda ambao utapigwa Jumanne, March 28 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Kampeni hiyo imeendeshwa leo ikimuhusisha Afisa Habari wa TFF Cliford Mario Ndimbo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, Afisa Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe na Afisa Habari wa Azam FC, Hashim Ibwe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wameshiriki kwenye kampeni hiyo ya kuhamasisha mashabiki wamenunua jumla ya tiketi 4000

Wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa klabu za Yanga, Azam Fc na Simba wameshiriki katika kampeni hiyo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.