Yanga yaanza mawindo ya TP Mazembe

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd March 2023


Yanga yaanza mawindo ya TP Mazembe

Baada ya mapumziko ya siku tatu, kikosi cha Yanga kimerejea mazoezini leo kuanza maandalizi ya mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya TP Mazembe. Mchezo huo utapigwa April 02 huko Lubumbashi katika uwanja wa TP Mazembe

Utakuwa mchezo wa kukamilisha ratiba Yanga ikiwa tayari imefuzu robo fainali ya michuano hiyo lakini Wananchi wanahitaji ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kumaliza wakiwa vinara wa kundi

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema wachezaji watashiriki mazoezi na kurejea makwao lakini March 27 wataingia kambini Avic Town kwa ajili ya kukamilisha maandalizi kabla ya safari ya DR Congo itakayokuwa March 30

Nyota wote ambao hawana majukumu ya timu za Taifa, wanashiriki program hizo za mazoezi. Wachezaji 12 wako katika majukumu ya timu za Taifa

Wachezaji walio kwenye majukumu ya timu za Taifa ni walinda lango Djigui Diarra (Mali), Metacha Mnata (Tanzania)

Mabeki Kibwana Shomari, Dickson Job, Ibrahim Bacca na Bakari Nondo Mwamnyeto (Tanzania)

Viungo ni Mudathir Yahya, Feisal Salum (Tanzania), Khalid Aucho (Uganda), Stephane Aziz Ki (Burkina Faso)

Washambuliaji ni Fiston Mayele (DR Congo) na Kennedy Musonda (Zambia)


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.