Yanga

Yanga yaanza mawindo ya TP Mazembe

Joel JJ By Joel JJ
23 Mar 2023
Yanga yaanza mawindo ya TP Mazembe

Baada ya mapumziko ya siku tatu, kikosi cha Yanga kimerejea mazoezini leo kuanza maandalizi ya mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya TP Mazembe. Mchezo huo utapigwa April 02 huko Lubumbashi katika uwanja wa TP Mazembe

Utakuwa mchezo wa kukamilisha ratiba Yanga ikiwa tayari imefuzu robo fainali ya michuano hiyo lakini Wananchi wanahitaji ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kumaliza wakiwa vinara wa kundi

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema wachezaji watashiriki mazoezi na kurejea makwao lakini March 27 wataingia kambini Avic Town kwa ajili ya kukamilisha maandalizi kabla ya safari ya DR Congo itakayokuwa March 30

Nyota wote ambao hawana majukumu ya timu za Taifa, wanashiriki program hizo za mazoezi. Wachezaji 12 wako katika majukumu ya timu za Taifa

Wachezaji walio kwenye majukumu ya timu za Taifa ni walinda lango Djigui Diarra (Mali), Metacha Mnata (Tanzania)

Mabeki Kibwana Shomari, Dickson Job, Ibrahim Bacca na Bakari Nondo Mwamnyeto (Tanzania)

Viungo ni Mudathir Yahya, Feisal Salum (Tanzania), Khalid Aucho (Uganda), Stephane Aziz Ki (Burkina Faso)

Washambuliaji ni Fiston Mayele (DR Congo) na Kennedy Musonda (Zambia)

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
26m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
29m ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
46m ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
49m ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
2h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
13h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →