Wayne Rooney nyota wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya Uingereza, amempongeza Harry Kane kwa kuvunja rekodi ya kupachika mabao kwenye timu ya Taifa
Kane alifunga moja na mabao ya Uingereza jana katika mchezo wa kuwania kufuzu Euro 2024 dhidi ya Italia Uingereza ikishinda mabao 2-1
Kane alifikisha mabao 54 akimpiku Rooney aliyekuwa akiongoza na mabao 53
"Pongezi kwako Kane kwa kufanikiwa kuwa mfungaji bora wa muda wote wa England. Nilijua haitachukua muda mrefu lakini umeivunja rekodi kwa haraka kuliko ilivyotarajiwa, nakupongeza Harry," alisema Rooney
Kane amehitaji mechi 81 tu kuvunja rekodi ya mabao 53 ya Rooney aliyoweka katika mechi 120
