Singida - DTB

Singida BS yampumzisha Dario hadi msimu ujao

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Mar 2023
Singida BS yampumzisha Dario hadi msimu ujao

Mmoja wa wachezaji waliokuwa tishio kwenye ligi kuu ya NBC mwanzoni mwa msimu ni pamoja na winga wa Singida Big Stars Dario Frederico

Dario aliuanza msimu kwa kasi kubwa akiisaidia Singida Big Stars kupata matokeo muhimu katika mechi za mwanzoni mwa msimu

Hata hivyo winga huyo raia wa Brazil baadae akakumbana na changamoto ya majeraha ya mara kwa mara hali iliyomfanya asionekane katika kikosi cha Singida BS

Dario alirejea kwao Brazil kwa ajili ya matibabu na Wanasingida hawatamuona tena katika mechi zilizosalia msimu huu

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Singida BS, nyota huyo amemaliza likizo ya mwezi mmoja liyokuwa amepewa na uongozi hata hivyo klabu imeamua kumuongezea muda wa mapumziko ili aweze kuwa imara zaidi

"Dario Frederico amemaliza likizo yake ya mwezi mmoja na ripoti ya daktari inaonesha amepona kwa zaidi ya 90%. Hata hivyo, klabu kupitia kwa ushauri wa kitaalamu wa daktari imemuongezea muda Dario ili aweze kuwa timamu kwa 100% apate na muda wa kutosha wa kupumzika"

"Kutokana na maamuzi haya, Dario atarejea rasmi wakati wa maandalizi ya ligi kuu msimu ujao wa 2023/24. Wadau na mashabiki wa Singida Big Stars watarajie kumuona Dario akiwa kwenye kiwango bora zaidi atakapoungana na timu kwenye kambi yetu ya Pre-season nchini Tunisia," ilisema taarifa ya Singida BS

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’