FT : Uganda 0-1 Tanzania

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th March 2023


FT : Uganda 0-1 Tanzania

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kimeibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Uganda katika mchezo wa kuwania kufuzu Afcon 2023

Bao pekee la Stars lilifungwa na Saimon Msuva kwenye dakika ya 68 akimalizia krosi murua kutoka kwa mlinzi wa kulia Dickson Job

Stars ilicheza kwa nidhamu kubwa katika mchezo huo ambao ulipigwa uwanja wa Suez Canal, huko Ismailia, Misri

Ushindi huo umeisogeza Tanzania mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi F baada ya kufikisha alama nne

Timu hizo zitarudiana tena katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Jumanne, March 28


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.