Azam - KMC

Azam Fc kujipima na KMC mechi ya kirafiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Mar 2023
Azam Fc kujipima na KMC mechi ya kirafiki

Wakati Ligi Kuu ya NBC imesimama kupisha kalenda ya mechi za kimataifa, Azam FC na KMC zinatarajia kukutana katika mchezo wa kirafiki utakaochezwa Jumatatu kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam

Taarifa iliyotolewa na Azam FC imesema baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 katika mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya JKU ya Zanzibar, wameamua kujiimarisha kwa kuendelea kujipima nguvu.

Awali Azam walitarajia kujipima na vigogo wa Kenya, Gor Mahia lakini mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa ulivunjika kutokana na machafuko ya kisiasa yanayoendelea Kenya

Jana KMC waliifunga Dar City inayoshiriki Ligi ya Championship mabao 8-0 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam

Katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam inakamata nafasi ya nne ikiwa na pointi 47 na katika hatua ya robo fainali ya Kombe la FA itacheza dhidi ya Mtibwa Sugar huku KMC yenyewe inapambana kujinusuru na hatari ya kushuka daraja

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
14h ago
READ MORE β†’