Sofiane Boufal na Abdelhamid Sabiri walifunga na kuipa Morocco ushindi wa 2-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil mjini Tangier Jumamosi usiku. Ulikuwa ushindi wao wa kwanza dhidi ya mabingwa hao mara tano wa dunia.
Wafuzu wa nusu fainali ya Kombe la Dunia Morocco walikuwa na kila sababu ya kuibuka na ushindi dhidi ya vinara wa soka Brazil katika mchezo wao wa kwanza wa nyumbani baada ya kampeni bora ya Qatar 2022.
Huku wakishangiliwa na mashabiki 65,000 katika uwanja wa Ibn Batouta mjini Tangier, Morocco walijaribu kumaliza mechi mapema lakini Brazil walisimama imara
Mechi ngumu iliyokuwa na matumizi makubwa ya nguvu, wachezaji wa Brazil wakilalamika vikali kwa mwamuzi baada ya msururu wa rafu za mabeki wa Morocco
Brazil walidhibiti mchezo huku Morocco wakiwa hatari katika mashambulizi ya kujibu ambayo yaliwahakikishia ushindi huo muhimu
Bao pekee la Brazil lilifungwa na Casemiro




