Chelsea

Vikwazo vya Abramovich vilivyoathiri Chelsea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Mar 2023
Vikwazo vya Abramovich vilivyoathiri Chelsea

Chelsea wanasema vikwazo vya serikali vilivyowekwa kwa mmiliki wa zamani Roman Abramovich vilichangia hasara ya klabu hiyo ya pauni milioni 121.3 ($148.8 milioni) kwa msimu wa 2021/22

Bilionea wa Urusi Abramovich aliwekewa vikwazo na serikali ya Uingereza mwezi Machi mwaka jana kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine

Alitajwa kama sehemu ya watu wa karibu wa Rais wa Urusi Vladimir Putin

Chelsea waliwekwa chini ya leseni maalum ambayo ilizuia uwezo wao wa kuuza tiketi, kukubali uhifadhi wa hafla na hata kusaini mikataba na wachezaji

Vikwazo hivyo vilibakia hadi Mei 30 mwaka jana wakati muungano mpya unaoongozwa na mfanyabiashara Mmarekani Todd Boehly ulipokamilisha kuinunua klabu hiyo

Chelsea ilisema katika taarifa Jumatatu kwamba mauzo yameongezeka hadi pauni milioni 481.3 kutoka pauni milioni 434.9 mwaka uliotangulia licha ya vikwazo hivyo

Mapato ya kibiashara yaliongezeka hadi pauni milioni 177.1. Matokeo ya kifedha hayahusu ununuzi wa Chelsea katika madirisha mawili ya uhamisho yaliyopita, wakati inaripotiwa kutumia takriban pauni milioni 600 kununua wachezaji wapya.

Matokeo ya 2021/22 yanaonyesha pauni milioni 118 ziliwekezwa kwenye kikosi cha wachezaji, ikiwa ni pamoja na mazungumzo ya sasa ya mkataba wa wachezaji, lakini faida ya pauni milioni 123 ilipatikana kwa mauzo ya wachezaji wakiwemo Tammy Abraham, Marc Guehi, Fikayo Tomori na Kurt Zouma.

Chelsea walisema waliendelea kuzingatia kanuni za fedha za UEFA na Premier League licha ya hasara na athari za vikwazo hivyo.

Klabu hiyo ilisema athari za vikwazo kwenye matokeo ya kifedha pia zitaonekana katika miaka inayofuata. Chelsea kwa sasa wako nafasi ya 10 kwenye jedwali la Premier League baada ya kuimarika hivi majuzi chini ya meneja Graham Potter

AFP

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
8h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
18h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
19h ago
READ MORE β†’