Ruvu - Mbeya City

Mbeya City yaichapa Ruvu Shooting 4-1, mechi ya kirafiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Mar 2023
Mbeya City yaichapa Ruvu Shooting 4-1, mechi ya kirafiki

Ruvu Shooting imekubali kipigo cha mabao 4-1 dhidi ya Mbeya Ciy katika mchezo wa kirafiki uliopigwa leo kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wenye lengo la kuziweka timu katika hali ya ushindani wakati huu ligi ikiwa imesimama kupisha kalenda ya CAF

Mbeya City inajiandaa na mechi yake ya robo fainali ya kombe la shirikisho, (ASFC) dhidi ya Singida Big Stars utakaopigwa Aprili 2, huku Ruvu Shooting wao wakijiwinda dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa ligi kuu utakaopigwa Aprili 9.

Maafande hao ambao wapo nafasi mbili za mkiani kwenye ligi kwa pointi 20 wameweka kambi yao jijini Mbeya

Mabao ya Mbeya City yamewekwa wavuni na Brown Mwankemwa dakika 16, Eliud Ambokile dakika ya 22, Richardson Ng'ondya dakika ya 77 na Baraka Mwalubanju dakika ya 88 huku la kujifariji kwa Ruvu likifungwa na Mgandila Shaban dakika ya 30.

Kocha mkuu wa Ruvu Shooting, Mbwana Makata amesema aliuhitaji mchezi huo ili kuangalia uimara wa kikosi chake kwa mchezaji mmoja mmoja na kwamba anaendelea kukisuka kabla ya mechi ijayo

"Makosa bado yapo tumekosa hadi penalti lakini pia tumefungwa, naendelea kupambana kuhakikisha nasahihisha upungufu ili mchezo ujao tuweze kushinda na kujiweka pazuri," amesema Makata.

Kocha msaidizi wa Mbeya City, Anthony Mwamlima amesema matokeo hayo yanawapa mzuka katika kujiwinda na mechi ijayo ya robo fainali dhidi ya Singida BS na kwamba msimu huu baada ya kukosa nafasi nne za juu kwenye ligi kuu, wanaelekeza nguvu kwenye ASFC.

"Malengo yetu ni kucheza kimataifa na inawezekana, japokuwa kwenye ligi kuu tumeshakwama hivyo tunaenda kupambania kwenye kombe la shirikisho kimsingi ni kufikia ndoto zetu," alisema Mwamlima.

Mwanaspoti

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
7m ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
4h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
5h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
6h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
7h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’