Kikosi cha Simba kitaondoka mkoani Kilimanjaro leo kuelekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca ambao utapigwa usiku wa kuamkia Jumamosi, April 01 2023
Simba iliondoka jijini Dar es salaam jioni ya jana Jumanne na kutua uwanja wa ndege wa KIA, lakini ndege yao ikapata hitilafu hivyo safari kuahirishwa
Meneja wa Habari wa Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema timu itaondoka Kilimanjaro asubuhi ya leo Jumatano



