Droo ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kombe la Shirikisho, itafanyika Jumatano ijayo April 05 huko Cairo, Misri
Simba ni miongoni mwa timu nane zilizofuzu robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa ikimaliza kwenye nafasi ya pili kutoka kundi C wakati watani zao Yanga wao wamefuzu robo fainali ya Shirikisho wakiwa na nafasi ya kumaliza kileleni mwa kundi D kutegemeana na matokeo ya mechi za mwisho
Mechi za kuhitimisha makundi zinapigwa mwishoni mwa wiki hii Simba ikimaliza mechi yake ya mwisho dhidi ya Raja Casablanca huko Morocco mchezo ukipigwa saa saba usiku wa kuamkia Jumamosi
Yanga itahitimisha mechi yake Lubumbashi DR Congo kwa mchezo dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa saa 10 jioni
Kwa mara ya kwanza Tanzania imeingia timu mbili kwenye robo fainali ya mashindano ya CAF



