Simba, Yanga tayari kwa droo ya robo fainali CAF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th March 2023


Simba, Yanga tayari kwa droo ya robo fainali CAF

Droo ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kombe la Shirikisho, itafanyika Jumatano ijayo April 05 huko Cairo, Misri

Simba ni miongoni mwa timu nane zilizofuzu robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa ikimaliza kwenye nafasi ya pili kutoka kundi C wakati watani zao Yanga wao wamefuzu robo fainali ya Shirikisho wakiwa na nafasi ya kumaliza kileleni mwa kundi D kutegemeana na matokeo ya mechi za mwisho

Mechi za kuhitimisha makundi zinapigwa mwishoni mwa wiki hii Simba ikimaliza mechi yake ya mwisho dhidi ya Raja Casablanca huko Morocco mchezo ukipigwa saa saba usiku wa kuamkia Jumamosi

Yanga itahitimisha mechi yake Lubumbashi DR Congo kwa mchezo dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa saa 10 jioni

Kwa mara ya kwanza Tanzania imeingia timu mbili kwenye robo fainali ya mashindano ya CAF


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.