Simba

Simba imepania ushindi Morocco

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Mar 2023
Simba imepania ushindi Morocco

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca ambao utapigwa usiku wa kuamkia Jumamosi

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari kulekea mchezo huo, Robertinho amesema wamefanya maandalizi ya kutosha kuelekea mchezo huo ambao malengo yake ni kusaka ushindi

"Tumekuja hapa kushindana, tumefanya maandalizi mazuri tukiwa na malengo ya kucheza vizuri na kupata ushindi," alisema Robertinho

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wa Simba, kiungo mshambuliaji Saido Ntibazonkiza amesema pamoja na changamoto ya uchovu unaowakabili, wamejiandaa vyema na watapambana ili kupata matokeo mazuri katika mchezo huo

"Tumekuwa na maandalizi mazuri, japo tuna uchovu wa safari, hiyo haiwezi kuwa sababu kwani wachezaji tunajua wajibu wetu tutapambana ili tupate matokeo mazuri," alisema

Simba iliwasili Morocco majira ya mchana ambapo baada ya mapumziko ya saa kadhaa Simba itafanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Mohammed V saa nne usiku kwa saa za Morocco ambapo Tanzania itakuwa saa saba usiku

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’