Singida - Mbeya - Ihefu - Yanga - Simba - Azam

Singida BS vs Mbeya City kuanza robo fainali FA

Joel JJ By Joel JJ
1 Apr 2023
Singida BS vs Mbeya City kuanza robo fainali FA

Robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) inaanza kutimua vumbi wikiendi hii, ambapo Singida Big Stars (SBS) inatarajiwa kuwakaribisha Mbeya City katika mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Liti, mkoani Singida kesho Jumapili

Mchezo mwingine utapigwa Jumatatu, April 03 Azam FC wakitarajiwa kuwakaribisha wakata miwa wa Manungu, Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi 

Ni mchezo wa kutoana jasho kutokana na umuhimu wa kila mmoja kutaka ushindi ili kusonga mbele hatua ya nusu fainali na hata fainali na kuchukua taji ambalo litawapa uwakilishi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Singida Big Stars ilitinga hatua hii baada ya kuwaondosha vinara wa Championship, JKT Tanzania kwa bao 1-0 mchezo uliochezwa mjini Singida. Mbeya City ilitinga hatua hii baada ya kuwaondosha Kagera Sugar kwa bao 1-0 katika mchezo wa hatua ya 16 bora uliochezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Mechi nyingine ambazo zitahusisha klabu za Simba na Yanga zitapigwa wiki ijayo

April 07 Simba itaumana na Ihefu Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru wakati April 08 mabingwa watetezi Yanga wataumana na geita Gold katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
4h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
7h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
7h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
8h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
8h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
8h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
8h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
9h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →