Timu nane zilizofuzu robo fainali Shirikisho Afrika

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd April 2023


Timu nane zilizofuzu robo fainali Shirikisho Afrika

Baada ya Yanga kuizamisha TP Mazembe kwenye dimba lao la nyumbani huko DR Congo kwa kuwachapa bao 1-0, US Monastir walipaswa kushinda angalau mabao matatu dhidi ya Real Bamako ili kuweza kuiondosha Yanga kileleni mwa kundi D

Monastir wakapata ushindi wa mabao 2-1 na hivyo kuihakikishia Yanga kumaliza kileleni mwa kundi  D wakiwa na alama 13

Yanga sasa itakuwa na faida kwenye hatua ya robo fainali kwa kuanzia ugenini na kumalizia mechi ya pili nyumbani

Yanga, AS FAR, Malumo Galants na ASEC Mimosas zimemaliza vinara wa makundi wakati US Monastir, Rivers United, USM Alger na Pyramids zimemaliza katika nafasi ya pili

Katika hatua ya robo fainali Yanga itamenyana na kati ya Rivers United, USM Alger au Pyramids

Droo ya mechi za robo fainali itafanyika siku ya Jumatano


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.