Klabu ya Simba imethibitisha wachezaji wake wawili Shomari Kapombe na Kibu Denis walipata majeraha kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca ambao ulipigwa nchini Morocco usiku wa kuamkia Jumamosi na Raja kuibuka na ushindi wa mabao 3-1
Taarifa iliyotolewa na Simba jana, ilibainisha kuwa wachezaji hao watafanyiwa uchunguzi wa majeraha waliyopata ili kuanza program za matibabu
Kapombe na Kibu wanaungana na winga Peter Banda ambaye pia atafanyiwa uchunguzi wa majeraha ya bega aliyopata wakati akiitumikia timu ya Taifa ya Malawi
Huenda nyota hao wakakosa mchezo wa robo fainali kombe la FA ambao Simba watacheza na Ihefu Fc April 07 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam
Simba inatarajiwa kurejea mazoezini siku ya Jumanne baada ya muda wa siku mbili za mapumziko ambao wachezaji wa timu hiyo walipewa baada ya kurejea kutoka Morocco



