Napoli wapigwa kama ngoma Serie A

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd April 2023


Napoli wapigwa kama ngoma Serie A

Mabingwa watarajiwa wa Serie A Napoli jana walipata kichapo cha tatu msimu huu wakibomolewa mabao 4-0 na mabingwa watetezi AC Milan

Vijana wa Luciano Spalletti wanaendelea kuongoza ligi mbele ya Lazio walio nafasi ya pili kwa tofauti ya pointi 16, huku Milan wakipanda hadi nafasi ya tatu

Rafael Leao alifunga bao la kwanza na Brahim Diaz akaifungia Milan bao la pili. Leao akaweka la tatu kabla ya lexis Saelemaekers akafunga bao la nne

Timu hizo zitakutana tena katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa mwezi huu, tarehe 12 na 18 Aprili

Napoli, ambao wamekuwa bora msimu huu, sasa wamepoteza michezo miwili kati ya minne iliyopita ya Serie A, baada ya kuchapwa katika mechi moja kati ya 24 za kwanza

Lakini bado wanahitaji kushinda mechi tano kati ya 10 zilizosalia za ligi ili kujihakikishia ubingwa wa Serie A tangu 1990

Hiki kilikuwa kipigo chao kikubwa zaidi tangu kufungwa 5-1 na Atalanta mnamo 2007-08


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.