Mlinda lango wa Yanga Metacha Mnata amejumuishwa katika kikosi bora cha wiki michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya mechi za raundi ya sita
Metacha alikuwa langoni wakati Yanga ikichuana na TP Mazembe katika mchezo uliopigwa huko Lubumbashi jana
Metacha alichaguliwa kuwa nyota wa mchezo huo akihakikisha Wananchi wanaondoka na ushindi muhimu wa bao 1-0 uliowafanya wamalize kileleni mwa kundi D
Hiyo ilikuwa mechi yake ya kwanza kucheza katika michuano hiyo akichukua nafasi ya Djigui Diarra aliyekuwa akitumikia adhabu ya kadi mbili za njano





