Azam Fc imekuwa klabu ya pili kutinga nusu fainali kombe la FA baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa robo fainali uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Licha ya kucheza pungufu kwa takribani dakika 60 baada ya Daniel Amoah kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi CHarles Ilanfya, Azam Fc bado ilikuwa bora mbele ya Mtibwa Sugar
Mabao ya Azam yalifungwa katika kila kipindi kuputia kwa Kipre Junior na Abdul Suleiman Sopu
Azam Fc imeungana na Singida BS kuwa timu za kwanza kutinga nusu fainali kombe la FA
Mshindi wa mchezo kati ya Simba dhidi ya Ihefu Fc atachuana na Azam Fc katika nusu fainali wakati mshindi wa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Geita Gold atachuana na Singida BS




