Yanga - Local

Mayele anaamini Yanga itatinga nusu fainali, Shirikisho

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 Apr 2023
Mayele anaamini Yanga itatinga nusu fainali, Shirikisho

Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele, amesema ubora wa kikosi chao unampa imani kubwa ya kufanya vizuri michezo miwili ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika na kutinga nusu fainali

Mayele amesema kitendo cha Yanga kufanikiwa kupata pointi kwenye michezo ya ugenini na nyumbani ni ishara nzuri na ubora wa kikosi cha timu hiyo na anaamini watasonga mbele zaidi katika mashindano hayo.

"Malengo yalikuwa ni makundi, lakini tumevuka huko na sasa tunaenda robo fainali, hii ni ishara nzuri kwetu kufanya vizuri na kucheza nusu fainali kwa sababu ya ubora wa kikosi cha timu pamoja na aina ya wachezaji tuliokuwa nao" alisema Mayele.

Aliongeza kuwa wanatambua umuhimu wa michezo iliyopo mbele yao na watafanikisha kila lemgo walilojiwekea na nguvu sasa wanazielekeza katika michezo iliyopo mbele yao hasa huo wa robo fainali.

"Sasa tumerejea nyumbani kujiandaa na michezo iliyopo mbele yetu ya Kombe la Shirikisho la Azam (FA Cup) na ligi kabla hatujacheza michuano ya kimataifa ya hatua ya robo fainali," alisema Mayele

Leo Yanga itafahamu timu itakayochuana nayo katika droo itakayofanyika huko Misri. Pyramids, USM Alger au Rivers United mojawapo itaangukia katika mikono ya Wananchi

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’