Manchester United imetangaza kumpa mkataba mpya wa miaka minne mlinzi wa pembeni Luke Shaw, mkataba utakaomuweka klabuni hapo hadi Juni, 30 2027
Beki huyo ameichezea klabu hiyo mechi 249 tangu ajiunge nayo akitokea Southampton mwaka 2014
Ameshinda mechi 29 za kimataifa akiwa na England, akishiriki michuano ya Kombe la Dunia na Euro
"Miaka tisa iliyopita, nilisaini klabu hii ya ajabu, na ninafuraha kuongeza muda wangu wa kukaa. Nimekua sana tangu nije Manchester miaka hiyo yote iliyopita, kama mtu na kama mchezaji"
"Najua nini kinahitajika ili kufanikiwa katika klabu kama hii. Tuko mwanzoni mwa safari yetu chini ya meneja na wakufunzi wake. Tayari tumefanikiwa msimu huu, lakini tunataka mengi zaidi. Kuna fursa nzuri ya kuunda kitu maalum hapa, na nitatoa kila kitu kuwa sehemu ya hiyo," alisema Shaw



