Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp amekiri timu hiyo iko kwenye hali mbaya na hakuna suluhu la haraka
Sare ya bila kufungana na Chelsea jana iliwafanya majgoo hao wa Liverpool kupoteza mwelekeo zaidi katika jitihada zao za kumaliza katika nafasi nne za juu za Ligi ya Premia
Katika mahojiano na talkSPORT baada ya mechi, Klopp alisema wako katika nyakati ngumu sana
"Kwa kweli ni hali mbaya ambayo hakuna mtu anataka kuwa ndani lakini sisi tumo. Hii si nchi ya ndoto yetu"
"Sina shida ya kuficha ukweli, pengine kwa sababu nazungumza hadharani watu ni wazi hukasirishwa na kufadhaika kuhusu majibu yangu na siwezi kubadilisha hilo"
"Hatuna suluhisho la haraka kwani kama lingekuwepo, tungerekebisha. Hii ndiyo hali yetu na inabidi tukabiliane nayo kwa njia yetu. Baadhi ya vilabu vinaishughulikia kwa njia tofauti na klabu yetu inataka kuifanya tofauti. Tunapaswa kufanya hivyo, haina shida hata kidogo, tutatoka hapa," alisema Klopp