Barcelona - Real Madrid - International

Benzema apiga hat-trik Real Madrid ikiinyoa Barcelona 4-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 Apr 2023
Benzema apiga hat-trik Real Madrid ikiinyoa Barcelona 4-0

Real Madrid imetinga fainali ya Copa del Rey kibabe katika uwanja wa Camp Nou baada ya kuifumua Barcelona mabao 4-0 katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali

Mshambuliaji Karim Benzema aliendeleza moto wake wa kuzifumania nyavu akiweka hat-trik akifunga mabao hayo baada ya Vinicius Junior kuitanguliza Real Madrid

Barcelona wameondoshwa katika michuano hiyo kwa kipigo cha mabao 4-1 wao wakipata ushindi wa bao 1-0 katika mechi ya mkondo wa kwanza iliyopigwa Santiago Bernebeu

Baada ya kupoteza mechi tatu mfululizo dhidi ya Barcelona, ni kama Real Madrid wamelipa kisasi cha machungu yote waliyopitia

Mashabiki wa Barcelona walikuwa wakiimba jina la Lionel Messi wakati wa wakifedheheshwa. Nyota huyo wa Paris Saint-Germain atashuhudia mkataba wake nchini Ufaransa ukimalizika mwishoni mwa msimu huu na inazidi kuwa wazi kuwa huenda asiongezee tena

Benzema alizima keleke za mashabiki wa Barca kwa hat-trick ya aina yake na kufanya mchezo huo kuwa kipigo cha mabao 4-0 na kuwaondoa kwenye michuano ya Copa del Rey

Mabao yake matatu pia yalimfanya kuwa mfungaji bora wa tatu wa El Clasico kwa Los Blancos, nyuma ya Cristiano Ronaldo na Alfredo Di Stefano

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
5h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
5h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
9h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
13h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
14h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
15h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
16h ago
READ MORE β†’