Real Madrid imetinga fainali ya Copa del Rey kibabe katika uwanja wa Camp Nou baada ya kuifumua Barcelona mabao 4-0 katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali
Mshambuliaji Karim Benzema aliendeleza moto wake wa kuzifumania nyavu akiweka hat-trik akifunga mabao hayo baada ya Vinicius Junior kuitanguliza Real Madrid
Barcelona wameondoshwa katika michuano hiyo kwa kipigo cha mabao 4-1 wao wakipata ushindi wa bao 1-0 katika mechi ya mkondo wa kwanza iliyopigwa Santiago Bernebeu
Baada ya kupoteza mechi tatu mfululizo dhidi ya Barcelona, ni kama Real Madrid wamelipa kisasi cha machungu yote waliyopitia
Mashabiki wa Barcelona walikuwa wakiimba jina la Lionel Messi wakati wa wakifedheheshwa. Nyota huyo wa Paris Saint-Germain atashuhudia mkataba wake nchini Ufaransa ukimalizika mwishoni mwa msimu huu na inazidi kuwa wazi kuwa huenda asiongezee tena
Benzema alizima keleke za mashabiki wa Barca kwa hat-trick ya aina yake na kufanya mchezo huo kuwa kipigo cha mabao 4-0 na kuwaondoa kwenye michuano ya Copa del Rey
Mabao yake matatu pia yalimfanya kuwa mfungaji bora wa tatu wa El Clasico kwa Los Blancos, nyuma ya Cristiano Ronaldo na Alfredo Di Stefano



