Yanga - Simba - Local

Waziri aiombea Yanga nafasi Super League

Joel JJ By Joel JJ
6 Apr 2023
Waziri aiombea Yanga nafasi Super League

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mohamed Mwinjuma amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF), Veron Mosengo-Omba

Katika mkutano huo ulifanyika leo Aprili 6, 2023 Durban nchini Afrika Kusini, Mwinjuma ametumia fursa hiyo kwa niaba ya Serikali kuiomba CAF iangalie namna itakavyoiwezesha Tanzania ikishirikiana na Kenya na Uganda kuandaa mashindano ya AFCON mwaka 2027 kwa pamoja.

Amesema hatua hiyo inatokana na mashindano hayo kutowahi kufanyika katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Aidha Mwinjuma amewasilisha ombi la Serikali la kuwa mwenyeji katika upangaji wa timu (droo) ya mashindano ya Super Cup pamoja na kuwa mwenyeji wa mchezo wa kwanza wa mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza mwezi Novemba, 2023 na kama ikitokea nafasi ya kuongeza timu basi CAF iipatie kipaumbele timu ya Yanga.

Katika mazungumzo hayo Mwinjuma pia amefikisha salaam za shukrani za Serikali ya Tanzania kwa CAF kukubali kuufanyia marekebisho Uwanja Benjamin Mkapa baada ya timu ya Simba kuchaguliwa kushiriki mashindano ya Super League.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa (CAF), Veron Mosengo-Omba ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano inaoutoa kwa maendeleo ya mpira wa miguu Barani Afrika akamhakikishia Naibu Waziri, Mwinjuma kwamba CAF itaendelea kushirikiana na Tanzania.

Ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuwa na utayari wa kuandaa mashindano ya AFCON ya Mwaka 2027 kwa pamoja na nchi za Uganda na Kenya.

Ametoa wito kwa nchi za Afrika Mashariki ziwasilishe maombi mapema kwa kuwa mashindano ya AFCON hayajawahi kufanyika katika ukanda wa Afrika Mashariki akibainisha kuwa maombi yameanza kupokelewa kuanzia Aprili 5, 2023 na yanatarajiwa kufungwa baada ya siku 21.

Kuhusu kuiongeza timu ya Yanga katika mashindano ya Super League Katibu wa CAF amemueleza Mhe. Mwinjuma kuwa kwa sasa wamechukua timu chache lakini baadaye Tanzania itaingiza timu mbili ambazo ni Simba na Yanga

Mwanaspoti

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
4h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
5h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
7h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
7h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
8h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
8h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
8h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
8h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
9h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →