Yanga - Geita Gold - Local

Geita Gold mikononi mwa Yanga robo fainali FA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Apr 2023
Geita Gold mikononi mwa Yanga robo fainali FA

Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga leo majira ya saa 2 usiku watashuka uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es salaam kumenyana na Geita Gold katika mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC)

Wakiwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Yanga inasaka ushinda ili kukata tiketi ya kutinga nusu fainali

Hata hivyo wanakutana na Geita Gold ambayo mara kadhaa imekuwa sio timu rahisi pale ilipokutana na Yanga

Mara ya mwisho Yanga na Geita Gold zilikutana hapohapo kwenye uwanja wa Azam Complex kwenye mchezo wa ligi kuu Wananchi wakiibuka na ushindi wa mabao 3-1

Geita Gold waliweka kambi ya takribani wiki moja jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo huo huku Afisa wao wa habari Hemed Kivuyo akitamba kuwa leo watalipa kisasi

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze alisema wachezaji wote wako tayari kwa mchezo huo, mlinda lango Aboutwalib Mshery ndiye mchezaji pekee ambaye atakosekana akiwa ni majeruhi

Mshindi wa mchezo huo ataungana na Singida BS, Azam Fc na Simba ambazo tayari zimetangulia nusu fainali

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
1h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
1h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
2h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
5h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
9h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
9h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
10h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
11h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
12h ago
READ MORE β†’