Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ameshinda tuzo ya Kocha Bora wa Ligi Kuu ya NBC kwa mwezi March 2023 wakati tuzo ya mchezaji bora ikienda kwa Jean Baleke
Katika mwezi Machi, mechi moja tu ya Ligi Kuu ilipigwa Simba ikiifumua Mtibwa Sugar mabao 3-0 Baleke akifunga hat-trik katika mchezo huo
Beleke amewashinda Daruweshi Saliboko wa KMC na Jeremiah Juma wa Tanzania Prisons
Robertinho ametwaa tuzo hiyo mbele ya Nasreddine Nabi wa Yanga na Abdallah Mohammed wa Prisons




