Yanga imetinga nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Geita Gold katika mchezo wa robo fainali uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Bao pekee la Yanga katika mchezo huo lilifungwa na Fiston Mayele aliyeingia kwenye kipindi cha pili
Kipindi cha kwanza Yanga walitengeneza nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia.
Mabadiliko yaliyofanywa na Kocha Cedric Kaze katika kipindi cha pili yaliinufisha Yanga
Yanga sasa imeungana na Singida BS, Azam Fc na Simba kwenye hatua ya nusu fainali
Kwenye mechi ya nusu fainali Wananchi watasafiri mkoani Singida kuwakabili Singida BS






