Yanga yaichapa Geita Gold 1-0, yatinga nusu fainali FA

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th April 2023


Yanga yaichapa Geita Gold 1-0, yatinga nusu fainali FA

Yanga imetinga nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Geita Gold katika mchezo wa robo fainali uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Bao pekee la Yanga katika mchezo huo lilifungwa na Fiston Mayele aliyeingia kwenye kipindi cha pili

Kipindi cha kwanza Yanga walitengeneza nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia.

Mabadiliko yaliyofanywa na Kocha Cedric Kaze katika kipindi cha pili yaliinufisha Yanga

Yanga sasa imeungana na Singida BS, Azam Fc na Simba kwenye hatua ya nusu fainali

Kwenye mechi ya nusu fainali Wananchi watasafiri mkoani Singida kuwakabili Singida BS


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.