Ihefu Fc wataweza kulipa kisasi kwa Simba?

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th April 2023


Ihefu Fc wataweza kulipa kisasi kwa Simba?

Leo Jumatatu April 10, Ihefu Fc ikiwa kwenye uwanja wake wa nyumbani Highland Estates, Mbarali huko Mbeya, itachuana na Simba katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Timu hizo zilikutana jijini Dar es salaam juzi kwenye mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) na Ihefu Fc kukubali kichapo cha mabao 5-1

Simba pia ilishinda kwa bao 1-0 mchezo wa duru ya kwanza wa ligi dhidi ya Ihefu Fc uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Ikiwa Mbarali, msimu huu Ihefu imejipambanua kuwa timu ngumu kufungika, je wataweza kuendeleza ubabe wao mbele ya Simba inayopigia hesabu ubingwa wa ligi kuu msimu huu?

Simba tayari imetua mkoani Mbeya ikiwa na kikosi chake kamili kikimjumuisha mshambuliaji Jean Baleke aliyefunga hat-trik katika mtanange wa FA

Ihefu Fc ilizifunga Yanga na Azam Fc hapo Real Estate lakini pasipo na shaka watakuwa na kazi kuweza kupata ushindi mbele ya Simba iliyoimarika chini ya Kocha Robertinho Oliveira

Ihefu wametangaza viingilio vya mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.