Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema pamoja na kuibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Ihefu Fc katika mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) uliopigwa uwanja wa Azam Complex juzi, wanatarajia kukabiliana na mechi nyingine tofauti dhidi ya Ihefu Fc huko Mbarali siku ya JUmatatu
Robertinho amesema ushindi waliopata Dar haupaswi kuwafanya 'wabweteke' kwani mechi ya pili dhidi ya Ihefu Fc itakuwa mpya na tofauti
"Ni kweli tumewafunga juzi lakini hii ni mechi nyingine, kuna dakika 90 mpya za kuthibitisha ubora uwanjani. Hata wao wataipitia mechi iliyopita kuona makosa waliyofanya na kujipanga upya nasi tumejipanga kutumia mbinu zetu kuhakikisha tunapata pointi tatu," amesema Robertinho
Simba ilitua Mbeya usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumatatu, April 10 katika uwanja wa Highland Estates
Kikosi cha Simba leo kitakamilisha mazoezi ya mwisho kuelekea mtanange huo ambao Simba inazihitaji alama zote tatu ili kuendelea kubaki katika mbio za ubingwa