KMC - Local

Kila goli KMC ni laki tano

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Apr 2023
Kila goli KMC ni laki tano

Mdhamini Mkuu wa KMC fc inayoshiriki Ligi kuu ya NBC Meridian Bet wameahidi kutoa kiasi cha Tsh 500,000/= kwa kila goli ambalo klabu hiyo itapata katika michezo ya ligi kuu iliyosalia

Lengo ni kutoa motisha kwa wachezaji kupambana zaidi na kukwepa mkasa wa kushuka daraja

Akizungumza na benchi la ufundi pamoja na wachezaji wa klabu hiyo Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo ya Meridian bet Bw. Matina Nkurlu, alisema kwamba lengo la zawadi hiyo ni kutoa motisha ili kuweza kuiweka timu kwenye mikono salama mpaka mwisho wa msimu

"Tumeamua kununua kila goli mtakalofunga kwa Tsh Laki Tano kwenye michezo yenu ya Ligi Kuu iliyosalia. Lakini jambo kubwa zaidi kiasi kitakacho patikana kitatumika kurejesha kwa jamii kwa sababu KMC ni timu ya Wanakinondoni na Watanzania wote," alisema

Kwa upande wa Nahodha wa KMC FC Emmanuel Nvuyekule alipongeza juhudi za Mdhamini wao na kuahidi kupambana zaidi

"Nimshukuru mwenyezi Mungu kwa kuwepo nanyi na kuzipokea taarifa hizi, lakini pia niwashukuru kwa kuja na wazo hili naamini hii itaongeza hamasa na kujituma kwenye timu yetu"

"Kubwa zaidi ni kwamba tuna muahidi mdhamini wetu kuwa tutafanya vizuri na tutafunga magoli mengi sana ili kusaidia jamii kwa wingi zaidi"

KMC imecheza michezo 25, imebakiza michezo 5 mkononi kabla ya Ligi kumalizika. Kwenye msimamo wanashika nafasi ya 12 wakiwa na pointi 26, Mchezo wao unaofuata ni dhidi ya Geita Gold.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’