Yanga - Kagera Sugar - Local

Maandalizi ya Kagera Sugar yamekamilika - Kaze

Joel JJ By Joel JJ
10 Apr 2023
Maandalizi ya Kagera Sugar yamekamilika - Kaze

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema maandalizi kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kagera Sugar ambao utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa Azam Complex, yamekamilika

Kaze amesema pamoja na muda wa maandalizi kuwa mdogo, ushiriki wao katika michuano mbalimbali uumewafanya kuwa tayari kucheza kila baada ya siku tatu

Kaze amesema anatambua mchezo dhidi ya Kagera Sugar utakuwa mgumu kwa kuzingatia ubora wa wapinzani wao

"Katika mechi ya kwanza tulicheza na Kagera Sugar kule Mwanza tukapata ushindi wa bao 1-0, walipata mkwaju wa penati lakini wakakosa. Nakumbuka ni moja ya mechi tulizopata usumbufu mkubwa. Hivyo tumejiandaa kikamilifu kuhakikisha changamoto hiyo haijirudii," alisema Kaze

Kaze amesema wanatarajia kuwa mabadiliko kidogo katika kikosi watakachotumia hapo kesho kulingana na utayari wa wachezaji

"Kwa sasa kikosi chetu kimeongezeka baada ya wachezaji waliokuwa majeruhi kurejea. Morrison (Bernard), Denis (Nkane) na hata David Bryson wote wamerejea"

"Morrison tutaendelea kumrejesha kikosini taratibu ili kuhakikisha hapati madhara, tukumbuke mechi yake ya mwisho ya ushindani kucheza ilikuwa Disemba 25 2022. Hivyo ni mchezaji muhimu lakini ataendelea kupewa nafasi kwa tahadhari," aliongeza Kaze

Nae winga Denis Nkane amesema wachezaji wote wako tayari kwa mchezo huo huku wakitambua wanahitaji kutimiza malengo yao ya kutwaa ubingwa

"Sisi kama wachezaji tunajua umuhimu wa mechi ya kesho hasa katika kujihakikishia tunatimiza malengo yetu ya kuchukua ubingwa, tuna imani tutafanya vizuri na kupata point tatu dhidi ya Kagera Sugar," alisema Nkane

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →