Manchester City - Bayern Munich - International

Manchester City vs Bayern Munich, UEFA CL

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Apr 2023
Manchester City vs Bayern Munich, UEFA CL

Mabingwa wa England na Ujerumani watakutana uwanjani Etihad siku ya Jumanne, wakati Manchester City wakiwakaribisha Bayern Munich katika mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League

Huku timu zote zikitakata kwene michuano hiyo, zimekabiliana na upinzani mkali kwenye ligi ya nyumbani

Man City iliifunga Southampton mabao 4-1 mwishoni mwa juma na kuendelea kuchuana na Arsenal katika mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza

Huo ulikuwa ushindi wao wa nane mfululizo. Mabao mengine manne mwishoni mwa juma yanamaanisha kuwa wamezifumania nyavu mara 31 katika kipindi hiki cha ushindi wa michezo minane.

Huku Erling Haaland akiwa kinara wa ufungaji, ana mabao 10 katika mechi sita tu za Ligi ya Mabingwa msimu huu, lakini Haaland hajawahi kufurahia mafanikio dhidi ya Bayern, ikipoteza mechi zote saba wakati akiwa na Borussia Dortmund.

Haaland alikuwa na mchango mkubwa kwa Man City katika kuwaona wakiendelea hadi hatua hii ya robo fainali, akifunga mabao matano katika kipigo kikubwa cha 7-0 dhidi ya  RB Leipzig, na kuthibitisha ushindi wa jumla wa 8-1 katika hatua ya 16 bora.

City walikutana na Bayern mara kadhaa katika miaka ya karibuni katika Ligi ya Mabingwa, wakishinda mara mbili kati ya mechi tatu walizokutana Etihad, huku kichapo chao pekee kwenye ardhi ya nyumbani kikiwa ni wakati Pep Guardiola alipokuwa ugenini na wababe hao wa Ujerumani

Licha ya kukaa kileleni mwa Bundesliga, Bayern hawako imara zaidi kama walivyo City nyumbani, pamoja na Thomas Tuchel kuanza vyema majukumu yake katika klabu hiyo akiirejesha kileleni mwa Bundesliga

Mechi ya kwanza ya Tuchel ilishuhudia Bayern wakiwashinda wapinzani wao wa taji Dortmund katika Uwanja wa Allianz Arena, lakini wakafuatia kwa kushindwa kwa mshtuko dhidi ya Freiburg, na kuondoshwa katika DFB-Pokal katika hatua ya robo fainali.

Wakarejesha ari ya ushindi wikiendi iliyopita na kujiimarisha kileleni mwa Bundesliga kwa tofauti ya alama mbili

Bayern wanalitaka taji la Ligi ya Mabingwa msimu huu, Tuchel aliisaidia Chelsea kushinda taji hilo mbele ya Manchester City msimu mmoja nyuma

Je atafanikiwa kuwaondosha tena kwenye michuano hiyo?

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
9h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
22h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’