Sadio Mane anadaiwa kumpiga Leroy Sane

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th April 2023


Sadio Mane anadaiwa kumpiga Leroy Sane

Sadio Mane aliripotiwa kumpiga mchezaji mwenzake wa Bayern Munich Leroy Sane mdomoni wakati wa mzozo katika vyumba vya kubadilishia nguo Jumanne usiku

Washambuliaji hao walionekana wakizozana uwanjani wakati timu yao ikiwa nyuma kwa mabao 3-0 kutoka kwa Manchester City katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa

Mzozo huo uliendelea hata baada ya mchezo kumalizika ambapo kulingana na BILD, wachezaji wenzao walilazimika kuwatenganisha Mane na Sane kwenye chumba cha kubadilishia nguo baada ya kushikana mashati

Bayern Munich bado haijasema lolote kuhusu tukio hilo lililoripotiwa

Kichochezi cha mzozo huo kinasemekana kuwa ni dakika ya 83 ambapo Sane alimlalamikia Mane kwa kupuuzia kile alichomuelekeza uwanjani


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.