Sadio Mane aliripotiwa kumpiga mchezaji mwenzake wa Bayern Munich Leroy Sane mdomoni wakati wa mzozo katika vyumba vya kubadilishia nguo Jumanne usiku
Washambuliaji hao walionekana wakizozana uwanjani wakati timu yao ikiwa nyuma kwa mabao 3-0 kutoka kwa Manchester City katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa
Mzozo huo uliendelea hata baada ya mchezo kumalizika ambapo kulingana na BILD, wachezaji wenzao walilazimika kuwatenganisha Mane na Sane kwenye chumba cha kubadilishia nguo baada ya kushikana mashati
Bayern Munich bado haijasema lolote kuhusu tukio hilo lililoripotiwa
Kichochezi cha mzozo huo kinasemekana kuwa ni dakika ya 83 ambapo Sane alimlalamikia Mane kwa kupuuzia kile alichomuelekeza uwanjani



