Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi, April 13 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Apr 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi, April 13 2023

Manchester City wanaongoza Real Madrid katika kinyang'anyiro cha kumnunua mchezaji wa Borussia Dortmund, Jude Bellingham baada ya Liverpool kujiondoa kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo huyo wa kati wa Uingereza mwenye umri wa miaka 19. (ESPN)

Mchezaji wa West Ham na Muingereza Declan Rice, 24, mchezaji wa kimataifa wa Ecuador mwenye umri wa miaka 21 Moises Caicedo, nyota wa Inter Milan na Italia Nicolo Barella, 26, na mchezaji wa Wolves na Ureno Matheus Nunes, 24, wamesalia kwenye orodha ya Liverpool inayomsaka kiungo mpya. (Florian Plettenberg)

Barcelona itazidisha hamu yao kumnunua Ilkay Gundogan baada ya kufurahishwa na mchezo wa kiungo huyo wa kati Mjerumani mwenye umri wa miaka 32 akiwa na Manchester City dhidi ya Bayern Munich kwenye Ligi ya Mabingwa. (Sport - kwa Kihispania)

Arsenal, Liverpool na Manchester United wanamfuatilia kiungo wa kati wa Bayern Munich na Uholanzi Ryan Gravenberch, 20. (Footmercato - kwa Kifaransa)

Tottenham, West Ham na Crystal Palace wote wanamtaka meneja Mholanzi Arne Slot, ambaye ameigeuza Feyenoord kuwa viongozi wa ligi ya Eredivisie. (Times- usajili unahitajika)

Arsenal wanalenga kumnunua winga wa Crystal Palace na Ufaransa chini ya umri wa miaka 21 th msimu wa joto, huku mchezaji huyo akiwa na thamani ya zaidi ya £40m. (Football Transfers)

Fulham, Aston Villa na Crystal Palace wanavutiwa na kiungo wa kati wa Besiktas na Ureno Gedson Fernandes, 24. (Calciomercato - kwa Kiitaliano)

Liverpool wametuma maskauti kumwangalia kiungo wa kati wa Fulham Joao Palhinha mara kadhaa wakifikiria kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 27 msimu wa joto. (Football Insider)

Timu ya wanawake ya Barcelona itajaribu tena kumsajili mshambuliaji wa Lyon na Norway Ada Hegerberg, huku timu hiyo ya Uhispania ikiwa tayari kutoa ada ya kuvunja rekodi ya dunia ya £420,000 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (90min)

Arsenal, Bayern Munich, Borussia Dortmund na Monaco wameonyesha nia ya kumnunua fowadi wa Crystal Palace na Ivory Coast h, 30, huku kandarasi yake ikikamilika msimu wa joto. (Footmercato - kwa Kifaransa)

Beki wa zamani wa Uingereza Chris Smalling, 33, atasaini mkataba mpya wa miaka miwili katika klabu ya Roma wiki hii licha ya nia ya kutakiwa na Inter Milan, Juventus na klabu kadhaa za Premier League. (i Sport)

Arsenal itadai pauni milioni 35 kwa mshambuliaji wa Uingereza Folarin Balogun, 21 ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo huko Reims na analengwa na RB Leipzig. (Florian Plettenberg)

BBC

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
27m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’