Real Madrid mguu mmoja ndani nusu fainali UEFA

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th April 2023


Real Madrid mguu mmoja ndani nusu fainali UEFA

Mabao ya Karim Benzema na Marco Asensio yaliihakikishia Real Madrid kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Chelsea katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya uliopigwa Jumatano usiku

Ushindi huo umeiweka Real Madrid katika nafasi nzuri ya kutinga nusu fainali kwani watahitaji matokeo ya sare hata kufungwa sio zaidi ya bao moja

Pamoja na kipigo hicho, mkufunzi wa muda wa Chelsea Frank Lampard amesema wachezaji wake wataendelea kuwa na imani kuwa wanaweza kufanya kitu nyumbani

AC Milan ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Napoli katika mchezo mwingine wa robo fainali uliohusisha derby ya Italia

Timu hizo zitarudiana tena wiki ijayo kwenye uwanja wa Diego Maradona huko Napoli


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.