Mshambuliaji wa Bayern Munich raia wa Senegal Sadio Mane anatarajiwa kuomba msamaha katika mazoezi ya Bayern Munich hii leo
Ni baada ya kitendo cha kumpiga Leroy Sane baada ya kipigo cha mabao 3-0 dhidi ya Man City siku ya Jumanne kwenye robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya
Viongozi wa Bayern walikutana jana na kujadili tukio hilo ambalo wanaona limeichafua taswira ya klabu hiyo
Mabosi wa Bayern wanazingatia adhabu mbalimbali kwa Mane ikiwa ni pamoja na faini, kusimamishwa kazi au kuondoka katika majira ya joto



