Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Yanga zimethibitisha kuwa mabingwa hao watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara, Yanga wamefanikiwa kumuongezea mkataba beki wao mahiri Dickson Job
Mkataba wake wa awali ulikuwa unamalizika mwishoni mwa msimu lakini sasa Yanga imefanikiwa kumshawishi na kumpa miaka mingine miwili
Yanga imekuwa katika mazungumzo na muda mrefu na Job lakini hakukuwa kumefikiwa makubaliano suala la mshahara likitajwa kuzitofautisha pande hizo
Afisa habari wa zamani wa Yanga Haji Manara amefichua kuwa mwafaka umepatikana na Job amesaini mkataba kuendelea kuitumikia Yanga
Yanga imeendelea kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambayo inaelekea ukingoni
Djigui Diarra, Yannick Bangala, Djuma Shabani, Mudathir Yahya, Bakari Nondo Mwamnyeto, Fiston Mayele, Farid Mussa, Zawadi Mauya ni miongoni mwa wachezaji ambao tayari mikataba yao imehuishwa