Chelsea italazimika kulipa zaidi ya euro milioni 100 kama wanataka kubadilisha mkopo wa Joao Felix kuwa uhamisho wa kudumu
Hayo ni kwa mujibu wa jarida la Uhispania la Marca, huku ikidai Atletico Madrid haitafikiria kumuuza fowadi huyo wa Ureno kwa chini ya kiasi hicho cha pesa msimu wa joto.
Felix aliondoka Atletico baada ya kutofautiana na meneja Diego Simeone, lakini ana mkataba na klabu hiyo hadi 2027.
Felix amekuwa na kiwango kizuri tangu alipowasili Januari Stamford Bridge na amekuwa mmoja wa wachezaji wa kuvutia zaidi wa The Blues, lakini bado hajaonyesha ufanisi wake kiasi cha kuwakilisha thamani inayotajwa akiwa na mabao mawili pekee katika mechi 13.
Marca wanadai Chelsea, hasa mmiliki wa Marekani Todd Boehly, wamefurahishwa na Felix na wako tayari kuketi kujadili uhamisho wake wa kudumu



