Yanga - Local

Kaze apiga hesabu alama tatu za ubingwa dhidi ya Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Apr 2023
Kaze apiga hesabu alama tatu za ubingwa dhidi ya Simba

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema wanatambua ugumu wa mchezo dhidi ya watani zao Simba lakini wamejiandaa vizuri na tayari kwa mchezo huo

Kaze amesema Yanga inakwenda katika mchezo huo ikiwa na kikosi chake kamili, ni mchezzaji mmoja tu, Aboutwalib Mshery ambaye ni majeruhi

"Tumejiandaa vizuri kwa mchezo huu mkubwa. Tunafurahi tunakwenda kwenye mchezo tukiwa na wachezaji wote isipokuwa mlinda lango Aboutwalib Mshery ambaye yuko anaendelea na matibabu"

"Hii ni mechi kubwa lengo letu ni kushinda. Wakati wa maandalizi tumefanya kila kitu muhimu kwa ajili ya mechi yenyewe kitu kikubwa ni kuwa na kiwango bora, tuweze kucheza vizuri na kupata matokeo mazuri"

"Umuhimu wa ushindi katika mchezo huu utatuweka katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa, hivyo hii ni motivation kubwa kwa wachezaji wetu," alisema Kaze

Kaze pia amesema kucheza na Simba kabla ya mchezo wa robo fainali ya kombe la Shirikisho dhidi ya Rivers United ni kitu kizuri kwao kwani itawapa mwanga wa nini watapaswa kufanya katika mchezo huo

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, kiungo Mudathir Yahya amesema wachezaji wote wamejiandaa na mchezo huo na wako tayari kupambana

"Wachezaji wote tumejiandaa vyema kupigania alama tatu. Hakuna presha yoyote tumejipanga na tutapambania ushindi," alisema Mudathir

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
3h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
13h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
14h ago
READ MORE β†’