Manchester City - Leicester - International

Haaland afikia rekodi ya Salah

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Apr 2023
Haaland afikia rekodi ya Salah

Erling Haaland alifikia rekodi ya mabao 32 ya Mohammed Salah Ligi Kuu ya Uingereza huku Manchester City ikizidi kuwasogelea viongozi Arsenal baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Leicester City Jumamosi jioni

John Stones aliwaweka mbele mabingwa hao watetezi ndani ya dakika tano za mwanzo kwa shuti la mbali likiwa bao lake la kwanza la ligi msimu huu

Mabao mawili ya Haaland katika dakika 20 zilizofuata yalimfanya afikishe jumla ya mabao 32, katika msimu wa mechi 38 wa Ligi Kuu akiifikia rekodi ya Mohamed Salah kwa Liverpool mnamo 2017/18

Haaland hakuweza kuivunja rekodi hiyo kwani alitolewa wakati wa mapumziko na Pep Guardiola kabla ya mechi ya robo fainali ya UEFA Champions League, ya mkondo wa pili dhidi ya Bayern Munich Jumatano.

Baada ya mabadiliko zaidi ya kocha huyo wa Man City, kasi ya mechi ilipungua na Leicester kurudisha bao kupitia kwa Kelechi Iheanacho dhidi ya klabu yake ya zamani na kuwapa hofu zaidi wapinzani wao.

Ushindi wa sita wa ligi mfululizo unaipa Man City pointi 70, huku kushindwa kwa timu ya Dean Smith katika mechi yake ya kwanza kuinoa Leicester kuwaacha Foxes nafasi ya 19, wakiwa na pointi 25

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
29m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
41m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’