Tetesi za usajili Ulaya Jumatatu, April 17 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th April 2023


Tetesi za usajili Ulaya Jumatatu, April 17 2023

Chelsea wamekutana na meneja wa zamani wa Bayern Munich Julian Nagelsmann wakati huu wakiendelea na harakati za kumtafuta kocha wao wa kudumu baada ya kutimuliwa kwa Graham Potter. (Athletic)

Kocha wa zamani wa Hispania Luis Enrique alisikitishwa kwa kuikosa nafasi ya kuwa meneja wa Chelsea kabla ya mechi ya kwanza ya robo fainali ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid, lakini anaonekana ni kocha anayepewa nafasi kubwa zaidi kwa sababu anaweza kusaidia kumsajili kinda wa Barcelona mwenye umri wa miaka 18, kiungo Gavi. (AS)

Real Madrid wanataka kutupia mwanya wa kipengele katika mkataba wa mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland mwenye umri wa miaka 22 kumsaini mshambuliaji huyo wa Norway katika msimu wa joto wa 2024. (Fichajes)

Arsenal wanataka kumnunua mshambuliaji wa Juventus Dusan Vlahovic mwenye umri wa miaka 23, huku mshambuliaji wa Everton Dominic Calvert-Lewin, 26, akiwa chaguo lao lingine kama watashindwa kumpata Mserbia huyo. (Football Insider)

Kiungo wa kati wa England Jude Bellingham, 19, angependelea kusalia Borussia Dortmund na kutathmini tena mustakabali wake mwaka 2024 kuliko kufanya uhamisho ambao haufai kwake msimu huu wa joto. (Athletic)

Mshambulizi wa zamani wa Liverpool Robbie Fowler anaamini Reds wako sahihi kutotumia sehemu kubwa ya bajeti yao ya uhamisho kwa Bellingham msimu huu wa joto kwani wanahitaji marekebisho makubwa katika sehemu yao ya kiungo. (Mirror)

Mshambulizi wa Napoli Victor Osimhen amekuwa akihusishwa na Manchester United lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria mwenye umri wa miaka 24 anaonekana kuwa ana furaha katika klabu hiyo ya Italia. (TG5 via Manchester Evening News)

Meneja wa Manchester City Pep Guardiola anashinikiza kuwabakisha kiungo wa kati wa Ujerumani Ilkay Gundogan, 32, na mchezaji wa Ureno Bernardo Silva, 28, katika klabu hiyo licha ya wachezaji wote wawili kuhusishwa na uhamisho msimu huu wa joto. (Football Insider)

Besiktas wanataka kumsajili tena mshambuliaji wa Uholanzi Wout Weghorst huku Manchester United ikiwa na uwezekano wa kubadilisha uhamisho wa mkopo wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 kutoka Burnley kuwa uhamisho wa kudumu. (Goal)

Kiungo wa kati wa Ujerumani Toni Kroos anatazamiwa kuendelea kusalia katika klabu ya Real Madrid kwa msimu mwingine, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 akiwa tayari kukubali kuongezewa mkataba katika klabu hiyo kubwa ya Hispania. (Marca)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.