Simba - Local

Tulistahili kupata ushindi mnono - Mgunda

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Apr 2023
Tulistahili kupata ushindi mnono - Mgunda

Kocha Msaidizi wa Simba Juma Mgunda amewapongeza wachezaji wa Simba kwa kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya watani zao Yanga katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jana

Mgunda amesema wachezaji walitekeleza maelekezo waliyopewa kwa usahihi na kama wangekuwa na bahati zaidi walistahili kushinda mchezo huo kwa idadi kubwa ya magoli

"Niwapongeze wachezaji wetu kwa ushindi huu. Tulijua ubora wa Yanga na madhaifu yao hivyo tulifanya maandalizi mazuri sana ya mchezo. Kocha (Robertinho) alituambia mapema tusiwape Yanga nafasi ya kuwa na mpira na tukiwa na mpira tuharakishe mashambulizi"

"Kipindi cha kwanza tulipaswa kufunga sio chini ya mabao manne lakini jambo muhimu tumeweza kushinda na niwapongeze wachezaji kwa kufanikisha ushindi huu," alisema Mgunda

Akizungumza kiwango cha mlinda lango Ally Salim, Mgunda alisema walimuandaa kucheza mechi hiyo kabla ya mchezo dhidi ya Ihefu Fc

"Niwaibie siri, tulimuandaa Salim kucheza leo (jana) kabla ya mchezo dhidi ya Ihefu. Baada ya mchezo ule tulimuambia atakuwa na jukumu kubwa la kukaa langoni kwenye mchezo huu"

"Nampongeza amefanya vizuri muhimu aendelee kujituma, umri wake bado mdogo ana nafasi ya kufika mbali zaidi"

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
41m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’