Arsenal - West Ham - International

Sare dhidi ya West Ham yamvuruga Arteta

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Apr 2023
Sare dhidi ya West Ham yamvuruga Arteta

Mikel Arteta amewalaumu wachezaji wake wa Arsenal kwa kushindwa kupata alama zote tatu dhidi ya West Ham katika kile ambacho kinaweza kuwa matokeo yenye athari katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza.

The Gunners walionekana kuwa katika hali nzuri katika mechi za ufunguzi kwenye Uwanja wa London Stadium walipopata uongozi wa mabao 2-0 ndani ya dakika kumi za kwanza

Gabriel Jesus na Martin Odegaard walifunga mabao ya The Gunners, hata hivyo, kwa mechi ya pili mfululizo walisalimu amri kwa mabao 2-0 kwa mkwaju wa penalti wa Said Benrahma na mkwaju wa Jarrod Bowen ukasababisha sare ya 2-2

Mechi hiyo pia ilishuhudia Bukayo Saka akikosa penalti wakati ambao ungeweka wageni mbele kwa mabao 3-1. Na Arteta hakufurahishwa na timu yake baada ya kupoteza uongozi wao wa mabao mawili

"Tulianza vizuri sana, Tulitawala mchezo, tulitawala uwanja na kufunga mabao mawili maridadi. Baada ya hapo tulifanya makosa makubwa kuacha kucheza tukiwa na malengo yale yale ya kufunga bao la tatu na la nne na tukifikiri tunaweza kucheza karibu nao na kudumisha matokeo na kuonekana rahisi sana"

"Tukawapa matumaini na wakaweza kurejea mchezoni. Kuna wakati mwingine ambapo unaweza kwenda mbele kwa mabao 3-1 baada ya dakika 50 na pengine mchezo umeisha"

"Dakika mbili baada ya hapo unakubali bao la kusawazisha. Hii ni sehemu ya soka. Wasiwasi wangu ni baada ya 2-0 kwamba tulifanya kosa hilo kubwa na hatukuelewa mchezo unahitaji nini kwa sasa," alisema Arteta

Baada ya matokeo hayo, uongozi wa Arsenal umepunguzwa na kubaki alama nne kileleni wakiwa pia wacheza mechi moja zaidi ya Manchester City inayoshika nafasi ya pili

Timu hizo bado hazijacheza mechi yao ya pili ambayo inaweza kuamua hatma ya ubingwa msimu huu

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
1h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
1h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
2h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
5h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
9h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
9h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
10h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
11h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
12h ago
READ MORE β†’